MAKAMU wa Rais,
Samia Suluhu Hassan
ameeleza kushitushwa na
idadi ya watoto wa kike
wanaopata mimba mkoani
Tabora na kuagiza hatua za
kuzuia tatizo hilo zichukuliwe haraka.
Alisema idadi ya mimba
za utotoni imeongezeka kutoka 21,889 mwaka 2017 hadi
mimba 27,390 mwaka 2018.
![Image result for mimba za utotoni](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgTMUy_bLA1jra7wqz5BylLb1bPrqfbZ09wyLSIY7L8VEJ4cMCjZaPXoIxVVuaUfraHh21FJsCxOQjg7p3m7BRs584ajq1N4B0SXOIgOhHfIrFt7XQcw0kF8b5XAyRUd7Wn68CeVRgXWDc/s1600/1.jpg)
Makamu wa Rais alitoa
kauli hiyo jana wilayani
Kaliua katika mkutano wa
hadhara uliofanyika katika
uwanja vya Kolimba.
Alisema kasi ya uwepo wa
mimba za utotoni ni kubwa na
haikubali na kutaka viongozi
mkoani Tabora kubadilisha
hali hiyo na kuwataka wazazi
wa- jitahidikuwalinda watoto wao.
Makamu wa Rais alieleza kuwa
wakati mwingine wazazi hawajitokezi kutoa ushahidi pale inapojulikana watoto wao wamepata ujauzito
na kwamba na kuongeza kuwa
vitendo hivyo ni kuwakatili maisha
yao.
Alisema kuwa hatua za makusudi
zisipochukuliwa kuna uwezekano
wa kuwa na wataalamu wa kike
wachache kwa sababu ya kushindwa
kutimiza ndoto zao.
Makamu wa Rais alipongeza
maandamano yaliyofanywa mkoani
Tabora katika kukemea na kudhibiti
mimba za utotoni akisema anatambua jitihada zinazofanywa na mkoa
kudhibiti hali hiyo.
Aliagiza jitihada zaidi ziongezwe
kwa vile kuna ongezeko kubwa la
mimba za utotoni mkoani Tabora.
Makamu wa Rais anaendelea na
ziara yake
mkoani
Tabora na
ametembelea wilaya
za Igunga,
Nzega,
Uyui na
Kaliua.