WAZIRI Mkuu,
Kassim Majaliwa amewahakikishia wananchi
kwamba ahadi zote
zilizotolewa na Rais John
Magufuli katika maeneo
mbalimbali nchini zitakuwa zimetekelezwa kwa
zaidi ya asilimia 90 ifi kapo
mwaka 2020.
Alisema Serikali ya
Awamu ya Tano imedhamiria kuwahudumia
wananchi na kuhakikisha huduma mbalimbali za kijamii
kama maji, afya, nishati,
elimu na miundombinu
zinapatikana kwa uhakika.
Alitoa kauli hiyo
alipozungumza na wananchi kwenye mkutano wa
hadhara uliofanyika katika
uwanja wa Kituo cha Polisi
cha Tarakea wilayani Rombo,
akiwa katika ziara ya kikazi
mkoani Kilimanjaro.
Waziri Mkuu alisema
wananchi waendelee kuwa
na serikali yao ambayo
imejipanga kutekeleza ahadi
zote zilizotolewa na Rais Magufuli kama Ilani ya Chama
Cha Mapinduzi (CCM) ya
2015-2020 inavyoelekeza.
Pia, Waziri Mkuu alisema
mtumishi mzembe, mwizi,
mla rushwa na asiyewajibika
hana nafasi katika serikali
ya awamu ya tano, hivyo
ametumia fursa hiyo kutoa
wito kwa watumishi wote
waimarishe utendaji wao.
Waziri Mkuu alisema kila
mtumishi wa umma anatakiwa ahakikishe anafanya
kazi kwa bidii ili kuiwezesha
serikali kutimiza lengo lake
la kuboresha maendeleo ya
wananchi kwenye maeneo
mbalimbali nchini hususani
ya vijijini.
“Iwapo watumishi wa
umma watatimiza majukumu yao ipasavyo changamoto nyingi zinazowakabili
wananchi kama upatikanaji
wa maji zitakuwa historia
kwa kuwa Serikali inatoa
fedha nyingi kwa ajili ya
utekelezaji wa miradi hiyo.
”
Waziri Mkuu alisema
kwa sasa serikali inatekeleza
Kampeni ya Rais Magufuli
ya kumtua mama ndoo kichwani, ambapo itahakikisha
kwamba wananchi wote
wanapata huduma ya maji
karibu na makazi yao.
Wakati huo huo, Waziri
Mkuu aliwaagiza viongozi
wa Halmashauri ya Wilaya
ya Rombo kwa kushirikiana
na Madiwani wahakikishe
wanaboresha masoko katika
mipaka ya Holili na Tarakea
ili yawe katika viwango vya
kimataifa.
Waziri Mkuu alisema
iwapo masoko hayo yaliyo
katika mpaka wa Tanzania
na Kenya yataboreshwa
yatawavutia na wananchi
wa Kenya kuja kufanya
biashara, hivyo kuiwezesha
halmashauri hiyo kuongeza
mapato.